Ona usajili wa akili YANGA. - TodayNews

Breaking

Thursday, 26 February 2015

Ona usajili wa akili YANGA.


  KLABU kongwe na tajiri katika Ligi Kuu Bara za Azam FC, Simba na Yanga kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa 2014-2015, zilitikisa kwenye usajili ambao kila mmoja akiamini amelamba dume.
Lakini baada ya wachezaji hao kuingia mzigoni, wapo wachezaji ambao unaweza kusema klabu hizo zililamba dume zilipokuwa zinasajili kutokana na namna waliosajiliwa walivyowasaidia na wanavyonogesha ushindi wa timu au uchezaji wake. Wachezaji wafuatao wamefanya kazi ya maana mpaka sasa;
Frank Domayo
Anaendesha gari aina ya Alteza. Ni kiungo wa Azam FC, alisajiliwa akitokea Yanga mwanzoni mwa msimu huu, lakini hakufanikiwa kucheza mechi zote za awali kwa sababu ya majeraha ambayo alifanyiwa upasuaji wa nyama za paja la mguu wa kushoto.
Lakini baada ya kupona na kurudi uwanjani, Domayo amekuwa mtamu kwa Azam kwa sababu ubora wake, umeongezeka maradufu.
Sasa ni mfungaji mzuri, analijua goli vizuri sana na sehemu ya mabao yake, yameitoa Azam kimasomaso. Kocha wake, Mcameroon Joseph Omog anajivunia uwepo wa Domayo kikosini hapo kuwa ni mhimili na ameifanya safu ya ushambuliaji ya kikosi hicho, kuimarika.
Hassan Ramadhani ‘Kessy’
Ni beki wa kulia wa Simba, yeye amesajiliwa katika dirisha dogo akitokea Mtibwa Sugar. Tangu atue kikosini hapo, Kessy amekuwa tegemeo kutokana na namna anavyofanya vizuri.
Ubora wake umedhihirisha hata anapokosekana ni pengo kikosini humo.
Umbo lake ni dogo lakini jamaa ni mtu wa kazi, ana kasi, nguvu na akili ya mpira, anaijua vizuri kuicheza beki ya kulia katika kupandisha mashambulizi na kukaba.
Simba haiwezi kujuta na sasa inajisifu kuwa imelamba dume.
Andrey Coutinho

No comments:

Post a Comment