PICHA 10 SIMBA WANAVYOIANDALIA DOZI MWADUI YA JULIO - TodayNews

Breaking

Thursday, 24 December 2015

PICHA 10 SIMBA WANAVYOIANDALIA DOZI MWADUI YA JULIO

IMG_0006
Wekundu wa Msimbazi Simba wameendelea kujifua kwenye uwanja wa chuo cha DIT jijini Mwanza kuelekea kwenye mchezo wake wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara dhidi ya Mwadui FC utakaochezwa December 26 siku ya Boxing Day.
IMG_0010
Simba itachuana na Mwadui kwenye uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga ikiwa ni baada ya kubanwa kwenye mchezo wao uliopita walipokutana na Toto Africans ya Mwanza.
IMG_0011
Kuelekea mchezo huo, Simba inakumbukukumbu mbaya kwani imetoa sare kwenye mechi mbili mfululizo wakati Mwadui FC yenyewe imeshinda michezo yake yote miwili iliyopita. Simba ilitoka sare dhidi ya Azam FC kwa kufungana bao 2-2 kwenye uwanja wa taifa, kisha ikatoka sare ya kufungana kwa goli 1-1 na Toto Africans.
IMG_0015
Mwadui yenyewe ilishinda kwa bao 2-0 dhidi ya Stand United kabla ya kupata ushindi mwingine wa goli 2-1 ilipocheza dhidi ya Ndanda FC.
IMG_0016
Simba inaweza ikawa na faida ya kumtumia kiungo wake mzimbabwe Justice Mabvi ambaye amejiunga na timu hiyo baada ya kugoma kusafiri na timu kufuatia matatizo kati ya uongozi na mchezaji huyo.
PICHA ZAIDI
IMG_0032IMG_0037IMG_0039IMG_0038

No comments:

Post a Comment