Timu ya Chelsea ilibidi wasubiri hadi dakika ya 49 kusawazisha goli kupitia kwa mshambuliaji wake mkongwe mwenye umri wa miaka 38 Didier Drogba,hadi mapumziko Chelsea walikua Yuma kwa goli moja lililofungwa na Marc Albraighton wa Leicester City.
Vijana hao wa Jose Mourinho waliingia kipindi cha pili kwa kasi ya ajabu na kumiliki mpira zaidi na kuwachukua takribani dakika nne kusawazisha goli hilo kabla ya kuongeza tena kupitia kwa kepteni wake John Terry na mwisho kabisa dakika ya 83 alikua ni kiungo Ramires aliepigila msumali wa mwisho.

Kwa matokeo hayo manaake ni kwamba ushindi dhidi ya Crystal Palace jumapili ijayo utakua umewahakikishia wazee wa darajani ubingwa wa msimu huu wa 2014/2015 na kufikisha point 80 ambazo hazitafikiwa na timu yoyote.
Leicester walioonyesha mchezo mzuri na kuongoza kipindi cha kwanza wanabaki nje ya kundi la kushuka daraja kwa pointi moja..
No comments:
Post a Comment